Free Thinking

Omnia mutantur nos et mutamur in illis Moyo ndi mabvuto

Saturday, 18 May 2013

Nini tafsiri ya ndoto hii?



Mwalimu Nkwazi Mhango
Naota nipo mitaa ya Mwitongo kule Butiama alipozaliwa na kuzikwa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Najihisi nikipiga ‘ulabu’ na jamaa zangu wa huko kabla ya kuondoka pale na kwenda zetu nyumbani kukamata ‘bukima’ na ‘msuli’ wa nyama au ‘inswi’ (ninaamisha ugali na mchuzi wa nyama au samaki).
Nikiwa narejea zangu home kutoka ulabuni, ghafla ‘ulabu’ wote unanitoka. Badala ya kuendelea kujiimbia wangu wa ‘ekerombeta n’ekerongo’ pombe zote zinaniishia.
Ninahisi mwili kunisisimka kana kwamba nitaona maajabu kama siyo balaa! Kujipa moyo na ithibati naamua kubadili wimbo. Najiimbia wimbo wa nyansuguta. Hili nalo halinisaidii.
Kwani mwili unazidi kunisisimka ikiwa ni dalili kuwa kuna jambo litatokea. Miili ya walevi kwa machale usipime. Na huu ni ukweli ambao naweza kuapia.
Maana bila ya kuwa na miili yenye ‘machele’ walevi wengi wangeishia ‘lupango’ kama siyo kufilisiwa na ‘ndata’ wakiwatoza uchache kwa kunywa pombe haramu.
Huwa nashangaa kuona ‘ndata’ haramu wakiwakamata walevi kwa kujinywea pombe wakidai ni haramu. Mbona hawakamati ‘lisirikali’ haramu linalokula rushwa na kuumiza walevi? Haya tuyaache.
Sitaki kuamsha hasira kiasi cha kwenda vituoni na kutembeza ‘makarate’ na ‘making-fu’ na ‘jet kune doo’ bure.
Ghafla, naona kaburi la tembo likinajisiwa na panya na vicheche aliowakaripia wakati wa uhai wake. Wana maya naye. Kwani aliwazuia kuirarua na kuinajisi ngozi.
Kila kinyama cha mwitu kiko pale kikifanya makufuru kwa kisingizio eti cha kumlilia tembo wakati ukweli ni kwamba vinamsimanga! Huu, kwa hivi vinyama, si msiba bali sherehe.
Vinasherehekea utadhani havitakufa! Hata kama vinaishi ni kimwili, kiroho vilijifia zamani gani! Ni bahati mbaya sana kwangu muota ndoto.
Nahisi hasira ikinipanda kiasi cha kukaribia kupasuka.  Najiuliza ndotoni kwa mshangao na uchungu: Amekosekana mwanaume wa kweli kwenda kuviangamiza vinyama hivi vichafu!
Tembo analia kwa majonzi hajililii, bali anawalilia swala na mbarapi aliowanya wasijirahisi na kuwaruhusu panya na vijinyama vya kiza wawatawale.
Fisi, mbwamwitu, nguchiro na vicheche wameshika kani. Maskini hayawani hawakumsikiliza wala kuelewa ujumbe wa maonyo yake!
Nani atawaokoa wakati huu walipozungukwa na vinyama vya kiza vyenye kila aina ya uroho na ulafi?
Anasikitika na kulia kwa vile hawakumuelewa. Waliingia `mkenge’ mchana kweupe hadi ikala kwao. Namuona mjane mtaua akilia. hajililii wala kumlilia mumewe wala watoto wake bali taifa la mahayawani wasiosikia wala kuhisi.
Hasemi. Ukikutana naye anatabasamu tabasamu la huzuni. Wajinga na wapumbavu huliona kama tabasamu la kweli wasijue ni kilio na unguliko! Tabasamu la mama huyu si la kweli hata kidogo.
Ana kinyongo, usongo, majonzi na ngoa. Atafurahia nini iwapo alimpoteza mume na kile walichotesekea?
Afurahie misiba ya kujitakia wa hayawani wanaoteseka wakimkumbuka mumewe na kumlilia aje kuwaokoa wakati kitabu chake kilishafungwa wasielewe?
Hili nalo linahitaji manabii kuja kuelezea? Mtakwisha msipoamka na kujipigania.
Naona nguruwe akijidai amejipaka uturi wakati anuka kinyesi kitupu. Harufu yake ni machukizo makuu sawa na matendo na tabia yake. Hana aibu wala akili. Kweli nguruwe ni nguruwe.
Ni hayawani mchafu na wa hovyo sina mfano. Anakwenda kwenye kaburi la tembo na kujifanya anamhani na kutoa heshima.
Tembo anakaribia kupasuka kwa hasira. Kwa vile hakuna mawasiliano baina ya wawili hawa, nguruwe anajiridhisha kuwa amempumbaza tembo na kumfurahisha ukiachia mbali kuwadanganya hayawani wenzake waliomzunguka wakimsifia upumbavu.
Nguruwe bila kujua anavyosanifika na wenye akili anahanikiza kujifisifu kuwa ametenda la maana. Ameridhika moyoni kuwa ameua ndege wawili, kumpumbaza tembo hata umma wa hayawani waliomwamini.
Naona machukizo ya kutisha. Ni bahati mbaya wengine wanayaona na kuogopa kusema wala kusimulia ndoto na uoni wao kama mimi. Sitanyamaza.
Nitasema hadi nipasuke kama siyo kutumiwa watu kunimaliza. Waovu na vinyama vya kiza hawapendi kusikia ndoto na mawazo yangu.
Kwani yanawaumbua na kuwaacha uchi. Wanaelewa vizuri ninachosema. Nyoyo zao zinawasonga. Wanatamani wanirarue kama siyo kuniteketeza wasiweze. Hata wakifanikiwa kunimaliza hawatamaliza mawazo na ndoto zangu.
Mie ni muota ndoto na kuota ndoto si kosa kama kunajisi vitakatifu.
Nikiwa natokwa na jasho najifunua na kuzidi kuota. Naona nguruwe mweupe akinajisi kila kitu. Amewaarika nguruwe wenzake kunajisi kila kitu. Anajishaua asijue tupo tunaotamani tumle lau aishie matumboni mwetu kwa hasira na chuki!
Naona nguruwe akitabasamu. Hii ni kawaida yake. Nguruwe ni mnyama asiye na aibu wala adabu. Hana akili wala busara zaidi ya hasara.

Tabasamu na tambo yake hata makufuru vinanifanya nihisi kibuhuti na hasira kiasi cha kutaka kumuua haramu huyu. Nawa moyoni na kujisemea:
Laiti hawa wanaogombea kuchinja wangemchinja huyu hayawani amani ikarejea duniani. Natamani niokote mawe na kumkong’ota huyu hayawani na kuvunja bufulu lake nisiweze.

Wenzake wamemzunguka hasa fisi wenye uchu wa nyama. Nitaanzia wapi wakati najiotea tu? Natamani ndoto hii ingekuwa ukweli lau niwateketeze vinyama hawa.
Naona kundi la bundi na kunguru wakiungana na hayawani wanajisi. Wanalizunguka kaburi la tembo wakiimba nyimbo za sifa ili kuwapumbaza swala wadhani lao moja wasijue ndiyo mwisho wa majaliwa yao. 
Kunguru wanaruka huku na huku wakiokota kila taka na manyoya ya tembo. Wanakenua utadhani watendacho ni sawa!
Nyoka wanafiki nao hawajivungi. Wanakuja na filimbi zao wakiimba nyimbo za sifa kwa nguruwe mpenda sifa.
Ametuna akitabasamu na kufaidi muziki wa kinafiki na kipumbavu. Laiti nguruwe huyu na wenzake wangejua kuwa kuna siku watalipa tena kwa bei mbaya huu uovu na makufuru wanayotenda, wala asingekenua na kufurahia kiama chake.
Nani amstue astuke hayawani huyu aso aibu na kidhabu?
Nikiwa naendelea kujiotea si wale nyoka waliacha kupiga filimbi wakajongelea kwangu! Ghafla niliamka na huku nikitweta kwa jasho ngoa na hasira!
Tuache utani. Tusipoamka kupambana, tutaishia kunajisiwa hai mithili ya tembo yule wa ndotoni.
Ni ndoto tu!

Chanzo: Nipashe Jumamomsi Mei 18, 2013.
Posted by NN Mhango at 06:57 No comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Friday, 17 May 2013

Kumbe ndiyo maana kuna migogoro kidini!

Posted by NN Mhango at 20:46 No comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Thursday, 16 May 2013

CCM kukacha midaharo: Ukihiyo na ukame wa mawazo?



Wengi wanakumbuka jinsi utawala wa sasa ulivyoingia madarakani kinamna.Hapa hatumaanishi kule kuchafuana na wizi wa fedha za umma Benki kuu (EPA) wala uchakachuaji. Watakumbuka kuwa rais Jakaya Kikwete, tofauti na mtangulizi wake, hakuna kitu anachokiogopa kama midahalo. Kwa vipindi vyote viwili alivyogombea, Kikwete alikuwa tayari kufanya loolote lakini siyo kushiriki midahalo. Ingawa hajawahi kueleza kwanini hakupenda kushiriki midahalo,hii imejenga dhana kuwa aliiogopa kutokana na kuwa na welewa mdogo wa mambo. Maana, wanaoamini hivyo wanasema kuwa kama angeshiriki angevuliwa nguo na ubovu wake kuonekana. Hivyo, kuepuka hilo, wanaongeza: Aliamua kuingia mitini kila alipoalikwa kwenye mdahalo.
Ushahidi mwingine ni kwamba tangu Kikwete aingie madarakani, hajawahi kwenda chuo kikuu kubadilisha mawazo na wanafunzi kama wenzake waliomtangulia walivyokuwa wakifanya. Hii kwa wachambuzi inaweza kutafsiriwa kama ukihiyo. Wapo wanaoshangaa jinsi Kikwete huyu huyu asiyependa mambo ya kisomi, alivyoridhika na kupenda kutumia udaktari wa heshima. Maskini ameonyesha ugumu wa kuelewa wanasema. Watangulizi wake wote walipewa shahada nyingi za heshima tena kuliko yeye. Lakini huwezi kusikia Dk Nyerere,Dk Mwinyi wala Dk Chinga. Ni Dk Kikwete pekee anayeweza kujisanifu bila kustuka.
Wakosoaji wake wanasema wazi: Kama kuna kitu Kikwete anapenda basi si kingine zaidi ya kuhudhuria maziko na kusafiri nje.
Hivi karibuni dhana hii ya kuogopa usomi ulipata mashiko pale iliposemekana Katibu mkuu wa CCM Abdulrahaman Kinana aliukacha mnyukano baina yake na Katibu mkuu wa CHADEMA Dk Wilibrod Slaa. Je Kinana alifuata mkumbo wa Kikwete au kuogopa kuvuliwa nguo hasa wakati huu anapokabiliwa na shutuma za kusafirisha pembe za ndovu na kuingiza na kuajiri wahamiaji  haramu nchini? Kwa habari zaidi BONYEZA hapa. Je watanzania wanawachukuliaje viongozi kama hawa wasiokuwa na mawazo bali dili? Tutafakari pamoja.
Wapo wanaosema kuwa kweli midahalo inawapiga chenga CCM. Hata hivyo,  wanawasukumiza kwenye kashfa na kuhujumu taifa na kusema kuwa CCM kwa hili hawana mpinzani.
Posted by NN Mhango at 18:39 4 comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Wednesday, 15 May 2013

Du hii kali Kenya yaongoza kwa uvumbuzi kurudi nyuma!

Ingawa toroli  linasifika hadi kuitwa ambulance, ukweli ni kwamba uvumbuzi huu haumsaidii mwananchi aliyetapeliwa na kuhujumiwa na wanasiasa. Wanapopata vitu kama hivi huridhika na kusahau kupambana na majambazi wenye madaraka waliowaahidi maisha bora wakaishia kuwapa maisha balaa. Hivi karibuni kulivumbuliwa toroli linaloitwa ambulance. Je ambulance ambayo injini yake ni binadamu inaweza kutuvusha? Inashangaza kwenye karne ya 21 Afrika inagundua nyenzo zilizotumika wakati wa ujima. Huwa najiuliza: Hawa akina mama wanaodhalilishwa kwenye mikokoteni kama mikungu ya ndizi wangekuwa wake wa wakubwa wangeshangilia janga hili linaloitwa uvumbuz? Je uvumbuzi huu ni hatua ya maendeleo au nyenzo ya kuwanyamazisha wanyonge na kuwafanya waridhike na mateso yao?
Posted by NN Mhango at 19:35 No comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Of First Families in Liberia and South Africa

Charles Sirleaf
Robert Sirleaf
Fumba Sirleaf
Duduzane Zuma


President Ellen Johnson Sirleaf received a big blow recently from her fellow Nobel winner, Leymah Gbowee. "I've been through a process of really thinking and reflecting and saying to myself 'you're as bad as being an accomplice for things that are happening in the country if you don't speak up,” Gbowee said. Gbowee was protesting Sirleaf’s act of appointing her three sons to oversee lucrative positions in her government. Apart from her son Charles, who is deputy governor of the Central Bank of Liberia, another son, Fumba is head of the National Security Agency. The third, Robert, is a senior adviser and chairman of the state-owned National Oil Company of Liberia
(NOCAL). Sirleaf ought to learn from Libya, Equatorial Guinea, Gabon, Congo, Egypt and Uganda where sons of presidents served in their fathers’ governments. It is sad for a democratically-elected- first-African-female president to set such a bad precedent.
 
Sirleaf a renowned academic promised to rule for one term. Later, she repudiated her own promise and ran for the second term. In 2009, the Truth and Reconciliation Commission of Liberia recommended that Sirleaf be barred from holding public office for 30 years for her role in supporting Taylor.  Sirleaf trashed the recommendations but apologized for backing Taylor.
 
When she was campaigning for presidency, she once asked to elected so that she could "bring motherly sensitivity and emotion to the presidency." Did she mean to become president and appoint her sons?
 
In law, we have offenses known as mala in se. those are crimes that everybody-- either enlightened or not—knows as opposed to crimes known as Mala prohibita which are those crimes that are prohibited by the Penal Code. This means. For the person of Sirleaf cabal and stature, it did not need any advice to know that appointing her own three sons in her government creates visible conflict of interests. Is Liberia becoming a clannish private estate for Sirleaf’s family?
The issue of the First family also played out in South Africa recently when an Indian plane carrying a wedding entourage landed at a military base near Pretoria contrary to the norm and law, irking many people in and outside South Africa.
The entourage was heading for a wedding between Vega Gupta and Indian born Aakash Jahajgarhia in the Sun City. Controversial as the Guptas are, they are business partners to Zuma’s son Duduzane, hence enjoying special treatment.
According to one South African political analyst, Fabian Scherer, the Zuma-Gupta marriage of convenience “… shows to what extent private businessmen, particularly with good relationship with the president and his family, have gained influence on South Africa’s parastatals.”
The Zuma-Gupta business alliance has baffled other countries that have hosted Zuma. In India, Mail and Globe quoted a source in Zuma’s entourage in India who intimated that Indian authorities were shocked with the great attention the Gupta’s were receiving.  “They were asked why the president is hanging around with these guys; they don’t have a great reputation in India.”
Justice Minister Jeff Radebe  expressed grave concern “… at this violation of the security protocol and total disregard of established practice for clearing the landing of aircraft in a military facility that is of strategic importance to the country.”
While the Guptas initially held that "The airplane had permission. No airplane in the world can land without permission." Atul Gupta however issued a general apology to all affected.
Though all is left for the government-cobbled commission to investigate, some major question any person can ask are: Is South Africa’s security reliable if anybody can just get into its territory and land at the military base without any detection?
Why didn’t the Guptas land at O Tambo International Airport? Did the plane have illegal items such as weapons, drugs, illegal immigrants and whatnot? Why did then pilot take such a risk considering that the plane would have been brought down had the military decided to intervene?
According to Mail & Guardian in a story that was run in 2012 accusing Zuma of benefiting from the Guptas, “There is evidence that the Gupta family is helping first lady number four, Bongi Ngema-Zuma, pay off her R3.8-million home loan.”
Zuma and his son ought to learn from the plights-cum-quandaries of Saddam Hussein, Muammar Gaddafi and Hosni Mubarak.  Will SA rid itself of the Gupta scandal?
Source: The African Executive Magazine May 15, 2015.  Ajay and Atul Gupta, and Sahara director, Duduzane ZumaDuduzane with his business partners, the  two brothers of Gupta family
Posted by NN Mhango at 04:28 No comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Tuesday, 14 May 2013

Hatimaye nimepata video ya MPIGS wa Kenya yaani wabunge!

Mwanaharaka Gacheke N Gachihi (pichani) mmojawapo wa walioanzisha vuguvugu la occupy parliament
Je wabunge wanaolala bungeni, kutukana, kukwepa vikao, kuongopa, kwenda kwa ajili ya sitting allowance siyo ma MPIGS? Je wabunge waliotumia vyeo vyao kuhongwa na wawekezaji hadi kupata pesa za kuficha Jersey Island na kuanzisha wizi kama EPA, Kagodamn, Dowans, IPTL, Songas, Meremeta na mwingine si ma MPIGS? Je wabunge walioingia bungeni kupitia uchakachuaji na wizi wa kura ukiachia mbali rushwa wakisaka rushwa na kutumia ubunge kama mtaji wa kujitajirisha si ma MPIGS? Sitashangaa kusikia siku moja kuwa kuna PIG President kama PIG anawakilisha uchafu uroho ulafi na kutoridhika. Je watoto wa wakubw wanaotumia madaraka ya wazazi wao siyo PIGLETS au vitoto vya nguruwe? Je nguruwe aweza kuazaa kondoo? Naomba tutafakari pamoja hasa kwa kufanya kile ambacho kitaalamu huita contents analysis based on Ethos and logos but not pathos. Karibuni nyote tutafakari kwa pamoja na kwa busara na akili kwa ajili ya kutafuta jinsi ya kulikomboa taifa letu after it went to the dogs.
Dokezo: Wale wanaokerwa na mawazo yangu wanisamehe kwa vile naamini nimeumbwa na kupewa ubongo na vipawa ili nifikiri hasa kwa ajili ya ukombozi wangu binafsi na kuibadili dunia yangu na wenzangu pale ninapoweza. Hiyo ndiyo falsafa yangu binafsi niiwekayo kwenye matendo au hadharani.

Posted by NN Mhango at 16:40 No comments: Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook

Je mbunge wako ni kati au sawa na hawa kwenye picha?